Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Motsepe Rais mpya CAF
Michezo

Motsepe Rais mpya CAF

Patrice Motsepe, Rais mpya wa CAF
Spread the love

 

MMILIKI wa klabu ya Mamelod Sundown Patrice Motsepe amechaguliwa kuwa Rais mpya wa shirikisho la mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) akichukua nafasi ya Ahmad Ahmad. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Motsepe amechaguliwa kuwa rais leo tarehe 12 Machi 2021, kwenye mkutano wa 43 wa Caf, uliofanyika jijini Rabat nchini Morocco ambao ulioudhuriwa na Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) Gian infantino.

Giann Infantino, Rais wa FIFA

Mkutano huo uliodhuliwa na wawaikilishi 54 kutoka kwenye mashirikisho ya mpira wa miguu barani Afrika ambao ndio wapiga kura kwenye uchaguzi huo huku Tanzania ikiwakilishwa na Wallace Karia ambaye ni Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF).

Katika uchaguzi huo Motsepe alikuwa mgombea pekee mara baada ya kukwama kwa rufaa ya Ahmad Ahmad ambaye alitaka kutetea kiti chake mara baada ya kufungiwa kujiusisha na soka kwa kipindi cha miaka miwili.

Ahmad Ahmad aliyekuwa Rais wa CAF

Mara baada aya kutangazwa kuwa mshindi kwenye uchaguzi huo Motsepe alimshukuru rais wa Fifa Gian Infantino na kusema kuwa “Tunaweza kutatua changamoto za Afrika kama tukiwa wamoja”

Jina la Motsepe kwenye mpira wa miguu ndani ya bara la Afrika lilianza kuonekana mwaka 2003 alipoinunua timu ya Mamelodi Sundown inayoshiriki Ligi kuu Afrika kusini.

Mamelod Sundown chini ya umiliki wa Motsepe imefanikiwa kutwaa taji la Ligi Kuu Afrika kusini mara tano mfululizo na kushinda taji la Ligi ya mabingwa barani Afrika mwaka 2016.

Licha ya kuwa mmiliki wa Mamelodi Sundown na Rais mpya wa Caf, Motsepe ni tajili namba tisa ndani ya bara la Afrika.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!