Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Moto waua wanafunzi 7 Kenya
Habari Mchanganyiko

Moto waua wanafunzi 7 Kenya

Spread the love

WANAFUNZI saba katika shule ya sekondari ya wasichana (Moi Girls High School) iliyopo Kibera, katika mji wa Nairobi nchini Kenya wamepoteza maisha baada ya moto kuzuka katika bweni, anaandika Hamisi Mguta.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu nchini humo, Fred Matiang’i ambaye alitembelea shule hiyo baada ya kutokea kwa tukio hilo, amesema leo mapema asubuhi  wanafunzi 10 waliojeruhiwa wamefikishwa katika hospitali ya Taifa ya Kenyatta.

Taarifa kutoka kwa Mkuu wa kituo cha Polisi wa Kibera, Enos Maloba imeeleza kuwa wanafunzi hao 10  walikuwa wakisumbuliwa na kushindwa kupumua kutokana na moshi uliotokana na moto huo lakini waliwahishwa hospitali.

Maloba amesema anaamini chanzo cha moto huo kimetokana na hitilafu ya umeme na kuongeza kuwa timu ya uchunguzi bado inaendelea kutafuta chanzo.

Hata hivyo, Matiang’i  amesema “Rais Uhuru Kenyatta ametuma wachunguzi kujua tatizo na kuwasilisha ripoti ya uchunguzi huo mwishoni mwa Semptemba 2, mwaka huu”.

Baadhi ya wazazi waliofika katika shule hiyo kutazama hali za watoto wao

Matiang’i amesema kuwa shule hiyo imefungwa kwa wiki mbili wakati uchunguzi ukiendelea na kuwa  wanafunzi wa kidato cha nne wataendelea na masomo yao ifikiapo siku ya Ijumaa na watasaidiwa kuendelea na masomo yao wakati ambapo wanajianda kufanya mtihani wa kidato cha nne wa KCSE.

Hata hivyo wazazi wamejitokeza kwa wingi kwenda kuchukuwa watoto zao baada ya mkuu wa shule hiyo kuwatangazia kuwachukua watoto hao.

Bwana Matiang’i aliandamana na gavana wa Nairobi Mike Sonko.

Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo mwanafunzi mmoja wa kidato cha kwanza ambaye alikuwa miongoni mwa wale waliotibiwa baada ya kisa hicho alisema kuwa moto huo ulianza saa saba usiku.

Alisema kuwa bweni lililochomeka lilikuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza na kwamba kulikuwa na makelele ya wanafunzi waliojaribu kujinusuru mbalii na mkanyagano huku wasichana wakijaribu kutoka ndani ya bweni hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!