Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Morrison Pasua Kichwa, asimamishwa kwa muda Simba
HabariMichezo

Morrison Pasua Kichwa, asimamishwa kwa muda Simba

Bernard Morrison akisaini mkataba wa kuitumikia Simba
Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya soka ya Simba umemsimamishwa kwa muda, kiungo mshambuliaji wake Bernad Morrison Raia wa Ghana kufuatia kuwa na matatizo ya utovu wa nidhamu aliouonesha kwenye kambi ya timu hiyo. Anaripoti  Mwandishi Wetu…(endelea)

Mchezaji huyo amesimamishwa kufuatia kuripotiwa kutoka kambini bila ruhusa kinyume na utaratibu uliowekwa na uongozi huo.

Taarifa ya ilitolewa hii leo tarehe 4 Februari 2022, na klabu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara ilieleza kuwa, mara baada ya Morrison kufanya hivyo, uongozi na benchi la ufundi ulimpa maelekezo ya kuwa asirejee kambini hapo mpaka atakapoonana na mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Barbara Gonzalenz.

Licha ya kupewa maelekezo hayo, mchezaji huyo hakuchukua hatua yoyote na hivyo kuendelea kukaa nje ya kambi ya timu hiyo, wakati kikosi hiko kikijiandaa na michezo mbalimbali ya Ligi Kuu na kombe la Shirikisho la Azam.

Sio mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kuripotiwa kuwa na matatizo ya utovu wa nidhamu, ikumbukwe alipokuwa anakipiga ndani ya klabu ya Yanga, alishawahi kuondoka kambini nyakati za usiku na kutokomea kusiko julikana na kisha kuibukia upande wa pili wa klabu ya Simba.

Mara baada ya kusimamishwa kwa mchezaji huyo uongozi wa klabu ya Simba umemtaka Morrison atoe maelezo kwa njia ya maandishi kwa mtendaji mkuu wa timu hiyo, na kama akikaidi kufanya hivyo uongozi wa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara umepanga kuchukua hatua kali.

Ikumbukwe mkataba wa mchezaji huyo kwa sasa unaelekea mwishoni, ukiwa umebakiza miezi sita toka aliposaini mwaka mmoja na nusu uliopita.

Morrison alisaini kuitumikia Simba katika kipindi cha miaka miwili kuanzia msimu wa 2020/21, mwezi Agosti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!