Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Morrison atemwa Simba
Michezo

Morrison atemwa Simba

Spread the love

WINGA raia wa Ghana anayekipiga klabu ya Simba, Bernard Morrison ameachwa kwenye kikosi cha wachezaji 24 kilichosafiri kwenda Harare Zimbabwe kucheza mchezo wa klabu bingwa Afrika dhidi ya FC Platinum. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kikosi hicho kimeondoka leo Ijumaa tarehe 18 Desemba 2020 majira ya saa 4:30 asubuhi kwa ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) huku kukiwa hakuna taarifa zozote zilizotolewa kuhusu kuachwa kwa Morrison.

Ni mara ya pili kwa Morrison kuwekwa pembeni kwenye kikosi cha Simba kinaposafiri kwenye michezo ya ugenini mara baada ya kuachwa kwenye safari ya Mbeya.

Simba ilikwenda Mbeya kucheza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mbeya City na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Morrison ambaye alijiunga na Simba akitokea Yanga kwenye dirisha kubwa la usajili, ameonekana kutopata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Simba tofauti na mategemeo ya wengi kutokana na ubora aliouonesha akiwa na Yanga.

Kikosi kamili cha Simba kilichosafiri kuelekea Zimbabwe kuchuana na FC Platinum tarehe 23 Desemba 2020, ni makipa Aishi Manula, Beno Kakolanya na Ally Salim, huku mabeki wakiwa Shomari Kapombe, Mohammed Hussein, Pascal Wawa, Ibrahim Ame, Erasto Nyoni, Gadiel Michael na Josh Onyango.

Kwa upande wa viungo ni; Jonas Mkude, Mzamiru Yassin, Said Ndemla, Hassan Dilunga, Rally Bwalya, Francis Kahata, Clotous Chama na Taddeo Lwanga.

Washambuliaji wakiongozwa Nahodha wao; John Bocco, Medie Kagere, Chris Mugalu, Miraji Athuman, Luis Miquisone na Ibrahim Ajibu.

Wachezaji wengine walioachwa kwenye kikosi hiko ni beki wa kati Kennedy Juma, Gerson Fraga ambaye ni majeruhi, Charles Ilamfya pamoja na David Kameta (Duchu) ambaye yupo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya vijana kilichopo Saudi Arabia.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!