Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Morrison apigwa rungu, kuikosa mechi ya Simba na Yanga
Michezo

Morrison apigwa rungu, kuikosa mechi ya Simba na Yanga

Spread the love

KAMATI ya uendeshaji na usimamizi wa Ligi (kamati ya Saa 72) imemfungia michezo mitatu mchezaji wa klabu ya Simba, Bernad Morrison na kumpiga faini ya Tsh. 500,000 mara baada ya kumpiga ngumi beki wa Ruvu Shooting, Juma Nyosso. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Morrison alifanya tukio hilo kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao Simba walipoteza kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Kwa mantiki hiyo mchezaji huyo atatumikia adhabu hiyo kuanzia mchezo ujao dhidi ya Mwadui FC siku ya Jumapili mpaka mchezo wa watani wa jadi utakao wakutanisha Simba na Yanga tarehe 7 Novemba, 2020.

Aidha kamati hiyo pia imemfungia michezo mitatu beki wa Ruvu Shooting, Juma Nyosso na kumtaka alipe faini ya Tsh. 500,000 mara baada ya kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Simba, Bernard Morrison.

Kwenye mchezo huo huo pia kamati hiyo imemtoza faini ya Tsh. 500,000 na kumfungia michezo mitatu mchezaji wa Ruvu Shooting, Shabani Msala kwa kosa la kumpiga teke Bernard Morrison.

Adhabu hizo zote zimetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 39(5) ya Ligi Kuu inayohusu uthibiti wa Wachezaji

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!