Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Michezo Mobetto amburuza mahakamani Diamond Platnum
Michezo

Mobetto amburuza mahakamani Diamond Platnum

Spread the love

NASEEB Abdul ‘Diamond Platnumz’ atakiwa kufika mahakamani Oktoba 30, 2017 kujibu malalamiko ya kushindwa kumuomba radhi mzazi mwenzake, Hamisa Mobetto na kushindwa kutoa matunzo ya mtoto, anaandika Mwandishi Wetu.

Diamond amepelekwa wito wa kuitwa mahakamani na mawakili wa Mabetto, Abdullah Zulu na Walter Godluck kutoka Kampuni ya Uwakili ya Century Attorneys.

Katika wito huo Diamond Platnumz anadaiwa kumdhalilisha na kutompa matumizi ya mtoto kwa takribani miezi miwili.

Zulu amesema mteja wao Hamisa Mobetto alimtumia Diamond notisi ya kumuomba radhi na kumtaka apeleke matunzo ya mtoto ndani ya siku saba.

“Baada ya kuona kimya tulipeleka kesi katika Mahakama ya Kisutu upande wa watoto (The Juvenile Court Of Dar es Salaam) na leo (Alhamisi) tumepewa barua ya wito na tayari mwanasheria wa mwanamuziki huyo ameipokea,” amesema.

Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Oktoba 30, mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

BiasharaMichezo

Wikiendi hii ushindi upo Meridianbet na si kwingine

Spread the love USHINDI huu ni wako mteja wa Meridianbet kama mechi...

BiasharaMichezo

Safari ya Gavi kutoka Academy ya Real Betis mpaka Barca

Spread the love  ANITWA Pablo Martín Páez Gavira ‘Gavi’, sasa ni mchezaji...

BiasharaMichezo

SBL yazindua Serengeti Oktoba Festival

Spread the love  KAMPUNI ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL) kupitia...

error: Content is protected !!