Saturday , 10 June 2023
Habari MchanganyikoTangulizi

Mo alikoroga

Mohamed Dewji 'MO Dewji'
Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu nchini na mwekezaji katika Klabu ya Simba, Mohamed Dewj ‘Mo’ ameanzisha mjadala mtandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tarehe 17 Septemba 2019, Mo aliweka ujumbe wake kwenye ukurasa wake wa twitter akisema ‘kuna maisha ya mtandaoni na maisha halisi.’

Kauli hiyo imepokewa kwa mtazamo tofauti ikizingatiwa kwamba, kutekwa kwake kulisababisha kuanzishwa kwa kampeni mtandaoni iliyokwenda kwa jina la ‘BringBackMo’.

“@moodewji Zamani nilizoea kusikia mipasho na kejeli kwa Mzee Yusuf siku hizi mipasho imeamia kwa viongozi wa siasa hadi soccer napita tu:” mchangiaji wa kwanza aliandika huku wengine wakifuata

Hata hivyo, baada ya ujumbe wake huo kwenye ukurasa wake wa twitter, Maria Sarungi ambaye ni mwanaharakati, ndiye aliyemchokonoa zaidi pale alipoandika ‘#BringBackMo ilikuwa maisha ya mtandaoni au maisha halisi?

Swali hilo liliwavuta wachangia wengi ambao baadhi yao walionekana kuwa na tafsiri zilizotofautiana, wengi wakionesha kutasiri ujumbe wa Mo kwa mtazamo hasi.

Mmoja wa wachangiaji wa twitter ya Sarungi alianza kwa kuhoji ‘Leo ndio tumekuwa “wa mitandaoni” lkn kumbuka kelele zetu ndio zilisaidia wewe kuachiwa na watekaji wako. Unless utuambie ule ulikuwa mchezo wa kutafuta umaarufu @moodewji.

Kutokana na jumbe mbalimbali zilizokuwa zikitolewa mtandaoni, Mo alirejea na kuomba radhi “Nisamehe sana dada yangu. Naona umeichukulia tweet yangu out of context. Narudia kuwashukuru wote ambao mliniombea ne kunisemea.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!