Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mnyika, Heche wang’ang’aniwa Polisi, Mdee asakwa
Habari za Siasa

Mnyika, Heche wang’ang’aniwa Polisi, Mdee asakwa

Spread the love

JOHN Mnyika, Naibu Katibu Mkuu (Bara) na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti, John Heche wamezuiliwa polisi kwa madai ya kuwa wameshindwa kufuata taratibu za dhamana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi hao wa Chadema pamoja na wengine walifika Kituo Kikuu cha Polisi kuitikia wito kama walivyotakiwa na jeshi hilo.

Walioachiwa kwa dhamana ni Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Salum Mwalimu na Dk. Vicent Mashinji.

Mwalimu amesema Mnyika na Heche wamebaki polisi kwa maelezo kuwa wamekuwa wakikwepa taratibu za dhamana.

Heche na Mnyika hawakuripoti polisi Machi 16, 2018 huku chama hicho kikieleza kuwa moja ya sababu ya wabunge hao kutoripoti ni kutokana na kuhudhuria vikao vya kamati za Bunge mjini Dodoma.

Mbali na kina Mnyika na Heche kuzuiliwa kutokana na kutoripoti polisi kama walivyotakiwa, leo Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Ester Matiko hawajafika kutokana na kupata dharura.

“Mdee yupo nje ya nchi kwa matibabu na Ester Matiko yuko Dodoma kwa shughuli za kibunge amechelewa usafiri,” amesema Dk. Mashinji.

Jeshi la Polisi wametoa amri ya kukamatwa kwa Mdee na Matiko popote walipo kwa kosa la kutoripoti polisi leo kama walivyotakiwa kufanya hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!