Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mlimani City watoa sababu za kufungia Nakumatt
Habari MchanganyikoTangulizi

Mlimani City watoa sababu za kufungia Nakumatt

Milango ya duka la Nakumatt likiwa imefungwa
Spread the love

DUKA kubwa (Supermarket) la Nakumatt lililopo jijini Dar es salaam, limelifungia, baada ya kukosa bidhaa za kutosha kwa muda mrefu pamoja na kudaiwa kodi za huduma mbalimbali, anaandika Angel Willium.

Meneja Mkuu wa Mlimani City, Pastory Mroso ameuambia MwanaHALISI Online, kuwa wamechukua uamuzi huo baada ya duka hilo kushindwa kutimiza vigezo walivyowekea ikiwa pamoja na kupewa notisi miezi minne kufanyia marekebisho tatizo hilo.

Mroso amesema pamoja na kuwapa notisi hiyo lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa, wakawaongezea tena notisi ya mwisho ya siku kumi ambayo ilikuwa inaisha siku ya Jumamosi, na kuamua kuwafungia asubuhi ya leo.

Meneja huyo ameendelea kwa kusema kwamba tatizo hilo limekuwa likiwaathiri wafanyakazi na hata bidhaa za wafanyabiashara wengine na wamelishalitolea taarifa serikalini kwa hatua zingine zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!