Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mlemavu wa macho ampa ushauri JPM 
Habari Mchanganyiko

Mlemavu wa macho ampa ushauri JPM 

Rais John Magufuli
Spread the love

MWALIMU Mkuu Mstaafu wa Shule ya Msingi Bwigiri Wasioona, Chamwino mkoani Dodoma, Sylivavus Hosea ambaye ni mlemavu wa macho, amemwomba Rais John Magufuli kuangalia namna ya kuteua wabunge watatu walemavu katika nafasi zake 10 za uteuzi. Anaripoti Dandson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na mtandao huu tarehe 17  Novemba 2019 amesema, pamoja na kuwapo wabunge wenye ulemavu bungeni, bado kuna nafasi za uwakilishi ambazo zinakosekana bungeni ikiwemo walemavu wa macho na wasiosikia (viziwi).

Kutokana na hali hiyo, amesema kama ikimpendeza Rais Magufuli na mwingine yeyote katika uongozi wake, aone jinsi ya kuchagua makundi hayo matatu yenye ulemavu kwa maana ya watu wenye ulemavu wa viungo, viziwi pamoja na wasioona.

Mbali na hilo amesema, jambo ambalo angefurahi kuona ni pale wabunge wangeweza kupeleka mswada bungeni ambao unawataka watu wenye ulemavu, kutokana na jumuiya za vyama vyao kama yalivyo makundi mengi ya vijana na wanawake.

“Zamani ilikuwa ngumu sana akina mama kugombea ubunge jimboni au udiwani katika kata, lakini kutokana na kupatiwa nafasi ya viti maalum na kufanya vizuri. Wameweza kuaminika hata kugombea majimbo na kufanikiwa kupenya na wakati mwingine kuwashinda wanaume,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!