KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars,’ Charles Boniface Mkwasa amepewa mkataba wa kudumu kukinoa kikosi hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu kuanzia Oktoba Mosi mwaka huu na kumalizika Machi 31, 2017.
TFF Imefikia makubaliano hayo na kocha Mkwasa baada ya kurudhika na utendaji wake katika kukinoa kikosi cha timu ya Taifa, ambapo mpaka sasa ameweza kuingoza Stars katika sare ya michezo miwili dhidi ya Uganda na Nigeria.
Kufuatia kusaini mkataba huo, Mkwasa atapatiwa huduma na marupurupu yote aliyokuwa akipewa kocha aliyeondoka.
Naye kocha Mkwassa ameeleza kufurahishwa na makubaliano haya na ameahidi kufanya kila jitihada kuhakikisha kiwango cha Timu ya Taifa kinapanda.
Aidha Kocha Mkwassa ametoa wito kwa wadau wa mpira kumpa ushirikiano katika majukumu yake mapya.
More Stories
Majaliwa aipongeza Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu
Biashara Mbeya Kwanza zaaga Ligi Kuu
Yanga yamaliza Ligi bila kufungwa