Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mkuu wa Wilaya aagiza waliotapeli mamilioni wawekwe ndani
Habari za Siasa

Mkuu wa Wilaya aagiza waliotapeli mamilioni wawekwe ndani

Pingu
Spread the love

MKUU wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gift Msuya ameagiza Jeshi la Polisi kuwakamata watu watatu wanaodaiwa kutapeli wananchi sita kiasi cha Sh. 6.5 milioni. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Watuhumiwa hao waliotambuliwa kwa majina ya Kulwa, Mayuga na Mang’ombe wanadaiwa kufanya utapeli huo tarehe 2 Novemba 2018.

Akizungumza baada ya kukutana na wakazi wa Igombe leo tarehe 5 Novemba 2018, Msuya amesema watu hao waliowarubuni wananchi hao, kwa kuwataka watoe fedha ili wakawasaidie kuwatolea dhamana baadhi ya watu waliokamatwa kwenye hifadhi ya Igombe.

“Kamanda OCS natoa maelekezo watu wote waliohusika kuwatapeli wananchi hawa hiyo milioni sita na nusu wakamatwe mara moja na wafikishwe kituo cha polisi,” ameagiza Msuya.

“Haiwezekani watu wengine wanaumia kutafuta hela kwa jasho, wengine wanakuja kula kwa mteremko. Mimi kama mtetezi wa wanyonge kama alivyo Rais wangu John Magufuli sitakubali jambo hili katika wilaya ninayoiongoza,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!