Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkuu wa Wilaya aagiza waliotapeli mamilioni wawekwe ndani
Habari za Siasa

Mkuu wa Wilaya aagiza waliotapeli mamilioni wawekwe ndani

Pingu
Spread the love

MKUU wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gift Msuya ameagiza Jeshi la Polisi kuwakamata watu watatu wanaodaiwa kutapeli wananchi sita kiasi cha Sh. 6.5 milioni. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Watuhumiwa hao waliotambuliwa kwa majina ya Kulwa, Mayuga na Mang’ombe wanadaiwa kufanya utapeli huo tarehe 2 Novemba 2018.

Akizungumza baada ya kukutana na wakazi wa Igombe leo tarehe 5 Novemba 2018, Msuya amesema watu hao waliowarubuni wananchi hao, kwa kuwataka watoe fedha ili wakawasaidie kuwatolea dhamana baadhi ya watu waliokamatwa kwenye hifadhi ya Igombe.

“Kamanda OCS natoa maelekezo watu wote waliohusika kuwatapeli wananchi hawa hiyo milioni sita na nusu wakamatwe mara moja na wafikishwe kituo cha polisi,” ameagiza Msuya.

“Haiwezekani watu wengine wanaumia kutafuta hela kwa jasho, wengine wanakuja kula kwa mteremko. Mimi kama mtetezi wa wanyonge kama alivyo Rais wangu John Magufuli sitakubali jambo hili katika wilaya ninayoiongoza,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!