Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mkuu wa shule, wanafunzi 79 watekwa nyara
Kimataifa

Mkuu wa shule, wanafunzi 79 watekwa nyara

Mji wa Bamenda nchini Cameroon
Spread the love

MKUU wa shule pamoja na wanafunzi wa kiume 79 wametekwa nyara na makundi ya waasi katika jiji la Bamenda nchini Cameroon. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo limetokea asubuhi ya leo tarehe 6 Novemba 2018, ambapo taarifa za awali zinadai kuwa, wahusika wa utekaji huo ni makundi ya wanamgambo wanaotaka kujitenga na nchi hiyo, hususan kwenye majimbo yanayotumia lugha ya kingereza.

Kwa mujibu wa video inayosambaa katika mitandao ya kijamii, inaonyesha wanafunzi hao wakirundikwa kwenye chumba kimoja bada ya kutekwa nyara, huku waasi wakiwaamuru kutaja majina yao.

Gavana wa jimbo la Kaskazini Magharibi, Adolphe Lele L’Afrique amevishutumu vikundi hivyo vya uasi, wakati serikali ikisema kwamba vyombo vya dola vinaendesha operesheni ya kuwakomboa mateka hao.

Chanzo: BBC Swahili

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!