Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mkutano wa Matiko waiponza Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Mkutano wa Matiko waiponza Chadema

Spread the love

JESHI la Polisi Wilayani Tarime mkoa wa Mara, wamewahoji viongozi watano wa chama cha Chadema wilayani humo, kwa tuhuma za kutoa lugha za uchochezi katika mkutano wa Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko uliofanyika jana tarehe 7 Aprili 2019. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Viongozi hao wa Chadema akiwemo Katibu wa Chadema mkoani Mara, Mwalimu Chacha Heche na  Katibu wa chama hicho jimbo la Tarime, Peter Magwi wamehojiwa leo tarehe 8 Aprili 2019 katika Kituo Kikuu cha Polisi wilayani Tarime cha Bomani.

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE, Magwi amesema wamehojiwa kituoni hapo kwa tuhuma za kutoa lugha za uchochezi na kuzidisha muda wa kufanya mkutano.

Magwi amesema wamekwisha maliza kuhojiwa na kwamba wanafuatalia taratibu za kupatiwa dhamana.

“Tumehojiwa kituo cha Bomani kuhusu mkutano wa jana wa Matiko, tuhuma tulizohojiwa ni kutoa lugha za uchochezi na kuzidisha muda wa mkutano,” amesema Magwi.

Mtandao huu ulimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoani Mara,  Henry Mwaibambe kwa ajili ya kupata taarifa zaidi za mahojiano ya viongozi hao wa Chadema kwa njia ya simu, lakini iliita pasipo kupokelewa.

Kwa taarifa zaidi kuhusu dhamana za viongozi hao, usikose kufuatilia mtandao huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!