Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkutano wa Mahakama ya Haki wafungwa
Habari Mchanganyiko

Mkutano wa Mahakama ya Haki wafungwa

Rais wa Mahkama ya Haki za Binaadam na Watu, Jaji Imani Aboud
Spread the love

 

MKUTANO wa kwanza wa kihistoria uliojumuisha mahakama ya haki barani Afrika na mbili za kikanda umemalizika leo kwa matumaini ya kupatikana msingi wa kuwezesha maamuzi ya mahakama hizo kutekelezwa na Serikali husika. Anaripoti Jabir Idrissa, Zanzibar … (endelea).

Akifunga mkutano huo kwenye Hoteli ya Verde, mjini Zanzibar, Waziri wa Sheria na Katiba wa Zanzibar, HAROUN ALI SULEIMAN alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inatambua mchango mkubwa wa mahakama hizo zikiongozwa na ile ya Bara la Afrika – Mahkama ya Haki za Binaadam na Watu – na inafurahi kuamua kuichagua Zanzibar kuwa mwenyeji wa kwanza wa mkutano huu.

Waziri Haroun ambaye ni mwanataaluma ya ualimu amesema Serikali inajali haki za watu wakiwemo wale wa makundi maalum na inachukua kila hatua kuhakikisha watu wote wanazifaidi haki hizo.

Ametilia mkazo umuhimu wa kuwepo mfumo mahsusi wa kuwezesha Serikali katika nchi wanachama wa mahkama hizo kutekeleza maamuzi yanayotolewa kutokana na kesi zinazofikishwa na wananchi wa barani Afrika.

Rais wa Mahkama ya Haki za Binaadam na Watu, Jaji Imani Aboud akitoa maelezo kabla ya kumkaribisha Waziri Haroun, amesema ana matumaini lengo la mkutano wao wa siku tatu limefikiwa na kwamba maazimio yaliyopo yataonesha dira ya kuondokana na utamaduni wa nchi wanachama kupuuza wajibu wa kutekeleza maamuzi ya mahkama hizo ambazo zimeanzishwa na mataifa yenyewe.

Mkutano huo uliofunguliwa Jumatatu na Rais wa Zanziber, Dk. Hussein Mwinyi, ulitanguliwa na mafunzo ya siku moja ya waandishi wa habari waliopo Zanzibar kuhusu historia ya mahkama hizo, utendaji wake na matatizo yanayowakabili.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa program maalum ya kuelimisha waandishi wa habari ili kueleza umma barani Afrika umuhimu wa mahkama hizo na kuhamasika kujitokeza kwa wingi kufungua mashauri kwa vile haki yoyote ni lazima ipiganiwe. Waandishi wapatao 30 walihudhuria mafunzo hayo.

Mahkama hizo zimekuwa katika mtihani wa maamuzi yake kusita kutekelezwa na hivyo kusababisha haki za watu kudharauliwa. Mahkama ya Afrika na ile ya Afrika Mashariki zina makao yake jijini Arusha, Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!