Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkurugenzi Jiji la Dar, ahamishiwa Kinondoni
Habari za Siasa

Mkurugenzi Jiji la Dar, ahamishiwa Kinondoni

Sipora Liana kuwa, mkurugenzi mpya wa Manispaa ya Kinondoni
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amempangia kazi, Sipora Liana kuwa, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam kuanzia leo Alhamisi, tarehe 25 Februari 2021. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea)

Sipora anakwenda kuchukua nafasi ya Aron Kagurumjuli, ambaye Rais Magufuli, alitengua uteuzi wake, tarehe 16 Februari 2021.

Rais Magufuli, amemteua Sipora siku moja baada ya kulivunja Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashuri ya Ilala kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, huku akieleza kwamba, watumishi wa Jiji la Dar es Salaam, lililovunjwa watapangiwa vituo vingine vya kazi.

Sipora alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaa, lililovunjwa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amesema, utaratibu wa kuwahamisha wafanyakazi katika vituo vingine utaendelea.

Aidha Waziri Jafo amemkabidhi Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Omary Kumbilamoto, gari lililokua likitumiwa na Meya wa Jiji lililovunjwa la Dar es Salaam.

Omary Kumbilamoto, Meya wa jiji la Dar es Salaam

Kumbilamoto, alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala iliyopandishwa hadhi kuwa Halmashuri ya Jiji la Dar es Salaam.

“Kama ilivyoelekezwa na Rais, watumishi watakuwa wanahamishiwa katika vituo vyao vya kazi. Katibu Mkuu Tamisemi nawaelekeza mfanye haraka kuwapangia vituo vya kazi,” amesema Jafo

“Gari alilokuwa anatumia Mstahiki Meya wa Jiji la awali likabidhiwe kwa Meya wa jiji jipya la Manispaa ya Ilala,” ameagiza Jafo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

error: Content is protected !!