Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkurugenzi awataka watendaji wake wajitathimini
Habari za SiasaTangulizi

Mkurugenzi awataka watendaji wake wajitathimini

Magesa Mafuru, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema
Spread the love

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Sengerema mkoani Mwanza, Magesa Mafuru amewataka watendaji katika ofisi ya Ofisa maendeleo ya jamii kujitathimini katika utendaji wao wa kazi kutokana na kutuhumiwa kutoa mikopo kwa vikundi kwa upendeleo kinyume na utaratibu. Anaripoti Moses Mseti … (endelea).

Mkurugenzi huyo ametoa kauli hiyo leo wakati akitoa hundi ya mikopo yenye thamani ya Sh. 42 milioni kwa vikundi 30 vya akinamama wilayani humo, fedha ambazo zinatokana na mapato ya ndani.

Amesema Halmashauri ya Sengerema ina kata 26 vijiji 71 vitongoji 419 na kila sehemu kuna akinamama ambao nao wanatakiwa kunufaika na mikopo inayotolewa na serikali ili wajikwamue kimaisha.

Amesema anashangazwa kuona kila mwaka vikundi vinavyopewa mikopo ni vile vile huku akidai watu walipewa dhamana hiyo ya kusimamia utoaji mikopo wakitoa kinyume na utaratibu.

Mafuru amesema utendaji kazi wa mratibu wa mfuko wa wanawake unatia mashaka hivyo anatakiwa kubadilika na kutoa fursa sawa kwa wanawake wote wilayani humo na kumtaka kujitathimi utendaji kazi wake.

”Siwezi kutoa mkopo tena, endapo hakutakuwa na vikundi vya akinamama wengine kutoka kata zingine, kila mikopo inatolewa hapa mjini tu inanitia mashaka tunapaswa kubadirika,” amesema Mafuru.

Mwenyekiti wa wanawake wajasiliamali, Halmashauri ya Sengerema, Daline Matonange amekiri kuwepo kwa madhaifu hayo huku akiwataka watendaji kubadilika juu ya suala hilo na kufuata maelekezo waliyopewa na mkurugenzi huyo.

Mratibu wa Mfuko wa Wanawake wajasliamali wilayani humo, Noela Yamo alipotakiwa kujibu tuhuma hizo, amesema yeye ni sehemu ya watumishi wa halmashauri hiyo anayetakiwa kuzungumzia swala hilo ni afisa maendeleo ya jamii na siyo yeye licha ya baadhi ya vikundi kumtupia lawama kuwa anatoa mikopo kwa upendeleo.

Kaimu Ofisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Sengerema, Boniphace Kasasilo amesema maelekezo yote waliyopewa watayazingatia na kuyafanyia kazi na kuondoa dosari zilizojitokeza na kuvitaka vikundi vinavyodaiwa kurejesha mikopo kwa haraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!