Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Mkude mikononi kwa Kamanda Kova
MichezoTangulizi

Mkude mikononi kwa Kamanda Kova

Jonas Mkude
Spread the love

 

KIUNGO wa klabu ya Simba J,onas Mkude kesho tarehe 5 Juni, 2021 atakwenda kujadiliwa mbele ya kamati ya nidhamu ya klabu hiyo, baada ya kuingia tena matatani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea). 

Mchezaji huyo ambaye toka Simba ilejee kutoka kwenye mchezo wa robo fainali dhidi ya Kaizer Chiefs, hajaonekana mazoezini, huku kocha wake Didier Gomes akidai kuwa na matatizo ya kifamilia.

Licha ya kocha huyo kunena hivyo, ukweli ni kwamba mchezaji huyo alifanya tena kosa la utovu wa nidhamu wakati timu hiyo ikiwa nchini Afrika Kusini.

Akitoa ufafanuzi juu ya swala hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Simba, Kamanda Mstaafu Suleiman Kova, alisema kuwa kamati hiyo inakwenda kukutana leo na kujadili suala lake.

Kamishna wa Polisi mstaafu Suleiman Kova, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu wa Simba

“Suala la Mkude limeshafika mezani na tutamjadili tarehe 5 (kesho), sisi kazi yetu ni kupokea malalamiko hata ikiwa mara ya pili na zaidi, akikubali kosa tuna muhukumu akikataa tunaita mashahidi wa upande wa ulalamikaji,” alisema Kamanda Kova.

Aidha kamanda Kova alisema kuwa mchezaji huyo atapewa haki yake ya kujitetea mbele ya kamati hiyo kwa kuwa wanazingatia uweledi katika majukumu yao.

“Tutafuta utaratibu ikiwa pamoja na kumpa haki zake za kujitetea tunafanya yote hayo kwa kuzingatia uweledi,” alisema Kova

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!