JEAN Bishikwabo (48) raia wa Kongo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa shitaka la kutakatisha fedha kiasi Sh. 14 bilioni, anaandika Faki Sosi.
Mtuhumiwa huyo mkazi wa Kinondoni Biafra, Dar es Salaam amepandishwa kortini leo na kusomewa mashitaka na Diana Mkondo Wakili wa Serikali mbele ya Respecious Mwijage Hakimu wa mahakama hiyo akidaiwa kujipatia fedha hizo kwa udanganyifu.
Katika kesi hiyo, mtu huyo anadaiwa kujifanya ni msambazaji na mnunuzi wa zao la korosho ambapo kati ya Oktaba 2015 na Januari 2016 na kujipatia kiasi cha Sh. 14 bilioni kwa njia ya udanganyifu kutoka katika Benki ya Biashara ya Afrika (Commercial Bank Of Africa).
Kutokana mashtaka hayo mtuhumiwa hakutakiwa kujibu chochote wala kupewa dhamana kutokana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kewsi zinazohusu utakatishaji wa fedha na uhujumu uchumi.
Mtuhumiwa huyo amerudishwa rumande na kesi hiyo inatarajia kutajwa tena tarehe 25 Agosti mwaka huu.
More Stories
Exim waadhimisha miaka 25, yapongeza wafanyakazi wake
NMB yamwaga vitanda, magodoro Kagera
NBC wasisitiza kukuza michezo, sanaa na utamaduni