RAIS Samia Suluhu Hassan amekitaka kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kujadili na kutoa kwa Serikali mapendekezo yanayotekelezeka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Ameyasema hayo leo Jumanne tarehe 5 Aprili 2022 awakati akifungua mktano wa kitaifa wa maridhiano, haki na amani ulioandaliwa na TCD.
“Mategemeo yetu kikosi kazi kipo kitakuja na yale mtakayojadili na matumaini yangu mtatuletea yale yanayotekelezeka, mkitupa mazito hatutayatekeleza na itabidi mnune na wanasema ‘gabage in, gabage out’ (ukiweka taka zitazoka taka) kwahiyo mkitutilia ‘gabage’ hapo zitatoka ivo ivo ‘gabage’ lakini mkiweka mazuri basi tutatekeleza vizuri,” amesema Rais Samia.
Mkuu huyo wa nchi ameitaka TCD kuzingatia hali halisi na mazingira ya Tanzania katika majadiliano yao.
“Nawaomba tuzungumzeni kwa mazingira yetu, hali yetu ya siasa, hali yetu ya uchumi na mazingira yetu ya kitanzania. Kama mimi nimetoa roho rahim kwenu nanyi rudisheni roho rahim.”
Amesema fursa ya kukutanana ni nafasi hadhimu ya kujadiliana na kufikia mwafaka wa kitaifa kama Watanzania.
“Niwaombe tutakayoyazungumza hapa tutazungumza kama watanzania. Tunapozungumza mardihiano tunazungumza vipi tunazungumza yapi tutakwenda mpaka wapi. tunaingia kwenye haki zetu kama watanzania ni zipi kama vyama vya siasa ni zipi na pale tulipofungua haki tuzungumze tutakavyoifungua, na tukitoka hapo sasa tunakwedna kudunmisha amani ya nchi yetu,” amesema na kusisitiza;
“Hakuna atakayetusaidia hapo , tutasaidiwa kukusanyika hapa, tutasaidiwa maposhona usfiri lakini haya matatu ni sisi…unapozungumza haki ujue haki yako inapoishia ya mwingine inaanza usije kujadili yako ukataka kubinya ya mwenzako, ” amesema.
Leave a comment