Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkewe Mbowe aeleza siri kanisa walilofungia ndoa
Habari za Siasa

Mkewe Mbowe aeleza siri kanisa walilofungia ndoa

Spread the love

 

MKE wa Mwenyekiti wa Chadema, Freema Mbowe, Dk. Lilian Mtei amesema Baba mkwe wake Aikael Mbowe ndiye aliyekuwa kiongozi wa ujenzi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Nshara ambalo lilitumika kufunga ndoa kati yake na mumewe miaka 30 iliyopita.

Amesema katika kanisa hilo lililopo Machame wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, alitambua kuwa limebeba historia kubwa ya familia ya Mbowe baada ya kufunga ndoa Agosti mwaka 1991. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika ibada ya shukrani iliyoendeshwa na Mchungaji Kelvin Kessy, Dk. Lilian amesema baada ya kujiunga na familia ya Mbowe miaka 30 iliyopita ndipo alipopata historia ya kanisa hilo na ukaribu wa familia hiyo.

Amesema kanisa hilo ambalo limevunjwa na  sasa linajengwa lingine kubwa, ndilo lililotumika kuwabatiza na kuwabariki watoto wao.

Aidha, akiomba waumini kuunga mkono familia hiyo ya Mbowe katika mchango Sh milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo, Dk. Lilian amesema kanisa hilo limebeba historia ya kipekee ya familia ya Mbowe.

“Ni kanisa ambalo lipo sana kwenye roho zetu ningeomba mtuunge mkono tuweze kulimazia hili kanisa na kutoa mfano kwa vizazi vijavyo.

“Sasa sijui uzao wetu nao watalivunja na wajenge lingine, itategemea watu watakuwa wameongezeka kiasi gani, licha ya kwamba halijakamilika lakini tumekaa ndani watu wengi… mtuunge mkono kuweka alama kwenye kanisa hili,” amesema.

Mbowe na msafara wake wameelekea Hai mkoani Kilimanjaro kwa mara ya kwanza baada ya kutoka gerezani walikodumu kwa zaidi ya miezi nane kabla ya kufutiwa kesi na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP). Mbowe na wenzake watatu walifutiwa kesi hiyo tarehe 4 Machi mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!