Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkandarasi wa barabara ‘awachefua’ Madiwani Morogoro
Habari Mchanganyiko

Mkandarasi wa barabara ‘awachefua’ Madiwani Morogoro

Mji wa Morogoro
Spread the love

MWENYEKITI  wa  Kamati ya Mipango Miji katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro,  Amir Nondo ameiomba iundwe kamati maalum kwa ajili ya kusimamia  barabara ya Mei Mosi kwa kuwa ujenzi wake umeshindwa kukamilika. anaandika  Christina Haule.

Nondo alisema hayo jana kwenye kikao cha kawaida cha baraza hilo ambapo ameliambia kwamba  Mkandarasi anayejenga barabara hiyo  kampuni ya Jassie Company Ltd, Building and Civil Engineering Contractor na kampuni ya ushauri ya M/S Dosh Ltd kwa sasa wamekimbia hazi na hawa[o eneo la mradi.

Aidha,  Nondo alisema, fedha za mradi huo zimetolewa  Benki ya Dunia na kwamba kati ya fedha hizo  zinaendelea kutumika katika kuboresha masuala mbalimbali ya kuleta maendeleo ya Manispaa.

Alisema ujenzi wa barabara hiyo ya Mei Mosi ulianza tangu Julai mosi 2015 ambapo ulitarajiwa kukamilika  Julai 30, 2016, lakini mpaka sasa bado haujakamilika.

“Sisi tumepata mradi mkubwa ndani ya Halmashauri 18  Tanzania zilizoomba huku tukiwa tumepata fedha nyingi  sasa doa hili tukilinyamazia litasababisha kukosa miradi mingine” alisema.

Amefafanua kwamba kamati hiyo  itakuwa na uwezo wa kupima kazi hata kwa kushirikisha msaada wa taasisi zingine za ukaguzi na kuona kama kweli ujenzi huo umeenda sambamba na mkataba uliopo.

Kwa uapnde wake, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro,  Pascal Kihanga aliahidi kujadiliana na kamati ya ujenzi na mipango miji na kuona namna ya kuunda kamati hiyo.

Aidha,  Kihanga alisema kuwa licha ya Mkandarasi huyo kutokuwepo kwenye eneo la mradi anaendelea kukatwa asilimia 10 ya hela yake kwa mwezi.

Kwa sasa alisema wamekusanya  kiasi cha Sh. milioni  293.7 ambazo zimekusanywa kwa miezi  saba na kuziweka kwenye akaunti ya Manispaa ambapo zitaingizwa kwenye shughuli zingine za maendeleo ya Manispaa hiyo kwa mujibu wa mradi wa Benki ya Dunia.

Naye Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini,  Abdulaziz Abood alisisitiza Halmashauri hiyo kuhakikisha fedha anazolipwa mkandarasi huyo zinaendana na kazi inayofanywa ili kuepuka hasara.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,  Michael Waruse alisema, fedha zinalipwa kwa mujibu wa sheria na mkataba uliopo na kwamba mkandarasi huyo hulipwa fedha kwa kazi anayoifanya.

Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa km 5.1 kwa kiwango cha lami unaogharimu Sh.  bilioni  11,805,176,469.00 ulishindwa kukamilika kwa wakati na kufanya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Bora na Serikali za Mitaa kutoa mwezi mmoja kukamilisha kazi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!