Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Miss Tz 2018 achomoza kinyang’anyiro ujumbe NEC-CCM
Habari za Siasa

Miss Tz 2018 achomoza kinyang’anyiro ujumbe NEC-CCM

Queenelizabeth Makune
Spread the love

 

MISS Tanzania 2018 – Queenelizabeth Makune ameteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kugombea nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kupitia Jumuiya ya vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Makune ambaye ni mzaliwa wa Shinyanga na msomi wa ngazi ya shahada ya uzamili katika usimamizi wa biashara (MBA) kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam atachuana na vijana wengine 13 kuwania nafasi tatu za Umoja wa Vijana wa CCM Bara (UVCCM).

Aliwahi kushinda mashindano ya ulimbwende katika vyuo vikuu Afrika (Miss University Africa) lakini pia ni mwanzilishi wa kampeni ya ‘Twenzetu Kutalii’ kufuatia kuteuliwa kwake na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kuwa Balozi wa Utalii wa ndani kwa miaka miwili kuanzia Mwaka 2018.

Makune alikuwa mrembo wa kwanza kupanda hadi kileleni mwa Mlima Kilimanjaro akiwa na wasanii. Pia alishiriki kikamilifu kwenye kampeni za urais mwaka 2020 na kundi la ‘Mama ongea na Mwanao’.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!