Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Miradi ya 18.75 trilioni yasajiliwa kwa mwaka mmoja
Habari Mchanganyiko

Miradi ya 18.75 trilioni yasajiliwa kwa mwaka mmoja

Spread the love

MIRADI ya uwekezaji 294 yenye thamani ya Dola za Marekani 8.12 bilioni (Sh. 18.75 trilioni), imesajiliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kuanzia Machi 2021 hadi Februari 2022. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 10 Machi 2022, jijini Dodoma na Waziri wa Uwekezaji, Dk. Ashatu Kijaji, katika mkutano wake wa kuelelezea mafanikio ya mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

“Kwa kipindi cha mwezi Machi 2021 hadi Februari 2022, Serikali ya Awamu ya Sita imevutia na kusajili jumla ya miradi ya uwekezaji 294, yenye thamani ya Dola 8.129 bilioni sawa na Sh. 18.75 trilioni,” amesema Dk. Kijaji.

Waziri huyo wa uwekezaji, amesema kwa mujibu wa takwimu za uwekezaji za 2020/2021, thamani ya miradi hiyo imeongezeka kutoka Dola 1 bilioni hadi 8.129 bilioni, ambayo itatoa ajira kwa Watanzania 62,301.

Amesema mafanikio hayo yanatokana na ushawishi kwa Rais Samia kwa wawekezaji, pamoja na makongamano ya biashara ya ndani na nje ya nchi, ambayo Serikali yake imeshiriki, ikiwemo la uwekezaji kati ya Tanzania na Kenya, lililofanyika Mei 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!