Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Miquissone, Wawa warejea kikosini dhidi ya Dodoma Jiji
Michezo

Miquissone, Wawa warejea kikosini dhidi ya Dodoma Jiji

Spread the love

 

KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Luis Miquissone pamoja na mlinzi wa kati, Pascal Wawa wamerejea kikosini baada ya kukosa mchezo uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Gwambina FC. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wachezaji hao wanarejea uwanjani kesho kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa saa 1 kamili usiku.

Akiongea mbele ya waandishi wa habari leo kuelekea mchezo huo wa kesho kocha msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kuwa wachezaji hao watakuwa sehemu ya kikosi kwenye mchezo wa kesho mara baada ya kukaa nje kwa kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano.

“Kwenye mchezo wa kesho tutamkosa Thadeo Lwanga ambaye alipata msiba wa dada yake, ila Pascal Wawa pamoja na Luis Miquissone wamerejea kikosini mara baada ya kumaliza adhabu zao za kadi tatu za njano,” alisema Matola.

Aidha kuelekea mchezo huo wa kesho kocha huyo, alisema kuwa wamejipanga vizuri na kuhakikisha kupata ushindi ili waendelee kutetea taji lao la Ligi Kuu Tanzania Bara ambao wao ni mabingwa watetezi.

Kwa upande wa nahodha msaidizi wa timu hiyo, Mohamed Hussein ameeleza kuwa wao kama wachezaji wamejipanga kuondoka na alama tatu kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Dodoma Jiji.

“Tupo uwanja wa nyumbani na tutautumia vizuri na makocha wameshatupa maelekezo yao jinsi gani tunavyotakiwa tucheze ili kesho tupate pointi tatu muhimu,” alisema nahodha huyo.

Simba inaingia kwenye mchezo wa kesho huku ikiwa kileleni kwenye msimamo wa Ligi hiyo wakiwa na pointi 58, huku nafasi ya pili ikishikwa na Yanga wenye pointi 57 na nafasi ya tatu wapo Azam FC wakiwa na pointi 54.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

error: Content is protected !!