Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Milioni 870 zakarabati Chuo cha Bustani, Profesa Ndalichako atoa neno
Elimu

Milioni 870 zakarabati Chuo cha Bustani, Profesa Ndalichako atoa neno

Spread the love
SERIKALI ya Tanzania, imetumia zaidi ya Sh. 800 milioni kukarabati Chuo cha Ualimu Bustani kilichopo Kondoa mkoani Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Hayo yamebainishwa leo Alhamisi tarehe 18 Juni 2020 na Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia aliyembelea chuo hicho kuangalia uboreshaji wa miundombinu.
Profesa Ndalichako amesema, Serikali imetoa kipaumbele kwenye sekta ya elimu kwa kurabati, kujenga miundombinu ya taasisi za elimu ikiwa ni pamoja na kununua vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili kuboresha dhana nzima ya ufundishaji na ujifunzaji.
Kuhusu  ukarabati na ujenzi unaoendelea kwenye vyuo vya ualimu, Profesa Ndalichako amasema, serikali inaboresha miundombinu  ya vyuo hivyo kwa awamu ambapo awamu ya kwanza imehusisha vyuo 10, awamu ya pili vyuo 8 na awamu ya tatu vyuo tisa na chuo cha Bustani kikiwemo na kufanya idadi  kufikia 27 kati ya 35 nchini nzima.
“Huu ni uwekezaji mkubwa ni vizuri miundombinu hii ikatunzwa kwa sababu serikali inatumia fedha nyingi kurudisha hadhi ya vyuo hivi.”
“Fedha iliyoletwa katika Chuo cha Ualimu Bustani Februari ni Sh. 874 milioni kwa ajili ya  kukarabati na kuongeza majengo mapya ambayo ni bweni, nyumba za walimu ikiwemo ya mkuu wa Chuo na kuongeza baadhi ya majengo kama Hosteli za wanafunzi wa kike,” amesema Profesa Ndalichako
Ametumia fursa hiyo, kuwataka wanafunzi kuwa wazalendo, kuipenda nchi yao,  kujitambua na huku wakiilinda tunu za Taifa zilizoachwa na waasisi wa nchi hii.
“Vijana uzalendo ni pamoja na kueleza mazuri yanayofanywa na serikali yenu, hata haya yanayofanyika hapa chuo cha Bustani, myaseme kwani hali ya miundombinu kabla ya ukarabati na baada ni tofauti sana  ni jukumu lenu kueleza mafanikio ya serikali ndani ya Taasisi zenu na hata nje,” amesema Profesa Ndalichako
Pia, ametumia fursa hiyo kuwatakia kila lakheri walimu tarajali wa mwaka wa pili wanaokwenda kuanza  mitihani ya elimu ya ualimu tarehe 29 Juni 2020.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Sezaria Makota ameishukuru serikali kwa namna ambavyo inapelekea miradi katika halmashauri ya Kondoa na hasa Chuo cha Ualimu Bustani na ujenzi wa ofisi za uthibiti Ubora wa Shule.
Amesema, miaka miwili iliyopita wizara ilipelekewa mradi wa maji ambao umekua msaada mkubwa kwenye  chuo hiko.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha ualimu Bustani, Joina Chanafi amemueleza Profesa Ndalichako chuo hicho kina jumla ya  watumishi wakufunzi 31 na kwamba hali ya utoaji elimu katika chuo hicho inaendelea vizuri bila changamoto yoyote.
Chanafi ameishukuru Serikali kwa kukarabati miundombinu ya chuo hicho ili kurejesha hadhi yake lakini pia kukiletea chuo  kwa wakati fedha za uendeshaji ugharamiaji wa maji, chakula na umeme.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!