MAAMBUKIZO ya virusi vya corona (COVID-19), duniani yamefikia milioni 128.8, waliopona milioni 103.9 na waliofariki dunia wakiwa milioni 2.8. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Marekani ni nchi inayoongoza kwa maambukizi duniani ikiwa na maambukizo milioni 31, waliofariki wakiwa 564,138 na waliopona ugonjwa huo wakiwa milioni 23.58
Brazili inashika nafasi ya pili kwa maambukizo milioni 12.66, waliopona wakiwa milioni 11 na waliofariki 317,936.
Nafasi ya tatu inashikwa na India ikiwa na maambukizi milioni 12.1, waliopona milioni 11.4 na waliofariki wakiwa 162.502.
Leave a comment