Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Michuano ya Kagame kuanza kutimua vumbi kesho
Michezo

Michuano ya Kagame kuanza kutimua vumbi kesho

Spread the love

MICHUANO ya klabu kwa ukanda wa Afrika Mashariki na kati (CECAFA Kagame Cup) yataanza kutimu vumbi rasmi kesho kwa jumla ya timu tisa kushiliki. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Katika ufunguzi wa michuano hiyo itapigwa michezo miwili ambapo mchezo wa afunguzi utakuwa kati ya Express ya Uganda dhidi ya Atlabara FC utakaochezwa majira ya saa 7 mchana, kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Mchezo wa pili, utawakutanisha klabu ya Soka ya Yanga ambao utapigwa majira ya saa 10 jioni, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, dhidi ya Big Bullet FC.

Kikosi cha Yanga

Timu hizo tisa zinazoshiriki michuano hiyo, zimegawanyika kwenye makundi matatu, ambapo kila kundi litakuwa na timu tatu.

Michuano hiyo pia itaendelea Agost 2, ambapo wawakilishi wengine kutoka Tanzania klabu ya Azam FC watashuka dimbani dhidi ya KCC kutoka Uganda, mchezo utakaopigwa Azam Complex Chamazi, huku mchezo wa kwanza utakuwa kati ya Message Ngozi na KMKM.

Michuano hiyo itafika tamati Agosti 14 kwa kupigwa mchezo wa fainali, majira ya saa 10 jioni kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!