Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mhubiri Paul Mackenzie, mkewe, wenzie 16 wafikishwa mahakamani
Kimataifa

Mhubiri Paul Mackenzie, mkewe, wenzie 16 wafikishwa mahakamani

Spread the love

MHUBIRI mwenye utata wa kanisa la Good News International lililopo kaunti ya Kilifi Malindi, Kenya na mkewe Rhoda Mackenzie pamoja na watuhumiwa wengine 16 wamefikishwa  katika mahakama ya Shanzu nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Mhubiri huyo na wafuasi wake  wanatarajiwa kufunguliwa mashtaka ya ugaidi baada ya mahakama ya Malindi Kaunti ya Kilifi kuwachilia huru na kisha kukamatwa tena ambapo hadi sasa Mackenzie anahusishwa na vifo vya watu takribani 100.

Uchunguzi wa miili ya watu hao umebaini kuwa huku njaa ikionekana kuwa chanzo kikuu cha vifo, baadhi ya waathiriwa wakiwemo watoto walinyongwa, kupigwa, au kukosa hewa.

Waendesha mashtaka wanaomba kumshikilia Mackenzie, ambaye alianzisha Kanisa la Good News International Church mwaka wa 2003, kwa siku nyingine 90 hadi uchunguzi utakapokamilika.

Jana Alhamisi Ezekiel Odero,mhubiri  maarufu wa televisheni  New Life International lililopo Mavueni Kaunti ya Kilifi, , aliachiwa huru kwa dhamana ya KSh. 1.5 milioni.

Odero pia atakuwa akisubiri rufaa aliyoikata ya kutaka huduma za Kanisa lake zilizozuiliwa ziweze kuendelea na Serikali iondoe zuio la akaunti zake za Benki ilizozifunga..

Awali, upande wa Mashtaka uliiomba Mahakama indelee kumshikilia Mchungaji huyo kwa siku 30 zaidi, ukidai unaendela kukamilisha upelelezi dhidi ya mtuhumiwa na kwamba uwepo wake nje unaweza kuharibu ushahidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!