Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mhagama akumbusha uzalendo watumishi wa Mashirika ya Kimataifa
Habari za Siasa

Mhagama akumbusha uzalendo watumishi wa Mashirika ya Kimataifa

Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu)
Spread the love

JENISTA Mhagama, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) ametoa wito kwa Watanzania wanaofanya kazi katika Mashirika ya Kimataifa kuitumia fursa hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya taifa lao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mhagama ametoa wito huo leo tarehe 15 Juni 2019 wakati akizungumza katika Kongamano la Nne la Tafa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililofanyika Jijini Dodoma.

Akitolea mfano wa Amon Manyama, Mkuu wa Programu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP), Mhagama amesema ni vyema Watanzania hao wakaiga mfano wake katika kutumia mashirika yao kuchochea ustawi wa Watanzania.

“Tunayo mashirika mbalimbali ya kimataifa yanayofanyakazi ndani ya taifa letu, na Watanzania wamepata fursa ya kutumikia mataifa hayo. Lakini kazi anayofanya Manyama kama muwakilishi kwa ustawi wa Watanzania ni kubwa sana,” amesema Mhagama na kuongeza:

“Labda tu nichomekee hapo, Watanzania wengine ambao wako katika mashirika mbalimbali ya kimataifa watusaidie kama kazi anayofanya ndugu yangu Manyama. Sisemi kama hawafanyi ila watufikishe kama anavyofanya Manyama.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!