Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Mhadhiri UDOM kizimbani kwa rushwa ya ngono
Habari

Mhadhiri UDOM kizimbani kwa rushwa ya ngono

Spread the love

JACOB Paul Nyangusi, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) nchini Tanzania, itamfunguliwa kesi ya Uhujumu Uchumi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), baada ya kukutwa na tuhuma za rushwa ya ngono. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Leo Alhamisi tarehe 13 Agosti 2020, Takukuru Mkoani Dodoma inamfikisha mhadhiri huo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, kujibu mashtaka yanayomkabili ya Uhujumu Uchumi kwa kosa la kutaka rushwa ya ngono.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo imetolewa leo na Sosthenes Kibwengo, Mkuu wa Takukuru mkoani Dodoma, Nyangusi amekwenda kinyume na kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007.

“Takukuru kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, tutamfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodom a Nyangusi (43) na kumfungulia shauri la Uhujumu Uchumi kwa kosa la kutaka rushwa ya ngono kinyume cha sheria,” inaeleza taarifa ya Kibwengo.

Chuo Kikuu cha Dodoma

Kwa mujibu wa taarifa ya Kibwengo, Takukuru ilimkamata Nyangusi usiku wa tarehe 3 Oktoba 2018 nyumbani kwake maeneo ya nyumba 300 jijini Dodoma, muda mfupi kabla ya kutekeleza nia yake ovu ya kufanya ngono na aliyekuwa mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza.

Tukio hilo lilitekelezwa na Takukuru baada ya taasisi hiyo kupokea taarifa kwamba mhadhiri huyo alimtaka mwanafunzi wake kingono kama sharti la kumsaidia ili aweze kufanya mitihani ya marudio na kumwezesha kufaulu katika somo lake.

“Na ndipo Takukuru ikaweka mtego na kumkamata. Baada ya uchunguzi kukamilika Ofisi ya Tiafa ya Mashtaka kuridhia kwa mujibu wa sheria ndipo mtuhumiwa anafikishwa mahakamani,” inaeleza taarifa ya Kibwengo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!