Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mgunduzi alama wenye ulemavu amwangukia JPM
Habari MchanganyikoTangulizi

Mgunduzi alama wenye ulemavu amwangukia JPM

Spread the love

 

JUTORAM Kabatele Mahala, ni Mtanzania aliyebuni alama sita za barabarani kwa ajili ya kuwalinda makundi ya watu wenye walemavu barabarani ambazo zinatumika kwa miaka kadhaa sasa. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Kabatele ni Baba wa familia ya mke mmoja na watoto wanne na licha ya mchango wake huo kwa taifa kutambulika na watu wachache, bado hajanufaika wala taifa halijatambua mchango wake kama muanzilishi wa kutumika kwa alama hizo.

Kwa sasa anaishi Vingunguti jijini Dar es Salaam ambapo Serikali ya mtaa ilimpa jina la mtaa huko anapoishi.

Mtaa huo unaoitwa Kabetele Street uliopo katika eneo la Mtambani, pia aliwahi kupata tuzo za mbunifu bora wa alama za barabarani kwa watu wenye ulemavu mwaka 2019 kupitia tuzo za ‘I Can Award’ aliyotunukiwa na marehemu, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi.

Lakini licha ya hayo yote, bado anataabika kwa ufukara huku alama zake zinatumika kwenye vitabu mbalimbali vya mafunzo ya usalama barabarani vyuoni na serikalini huku akimwomba Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli amsaidie.

Fuatilia mahojiano yake na MwanaHALISI TV .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!