Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Mgunda kuiongoza Simba Ligi ya Mabingwa Afrika.
HabariMichezoTangulizi

Mgunda kuiongoza Simba Ligi ya Mabingwa Afrika.

Spread the love

 

Klabu ya Soka ya Simba imemtangaza Juma Mgunda kuwa kocha wa muda wa klabu hiyo atakayesaidiana na Seleman Matola, kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Nyassa Big Bullet ya nchini Malawi. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Mchezo huo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa utapigwa tarehe 10 Septemba 2022, ambapo Mgunda atakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachosafiri hapo baadae kuelekea nchini Malawi.

Taarifa ya klabu ya Simba ilitolewa usiku wa jana septemba 7 mwaka huu, muda mchache mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Kmc imekeza kuwa, Mgunda ni kocha mwenye leseni A ya Shirikisho la soka barani Afrika (CAF), na hivyo kukidhi vigezo vya kuiongoza timu hiyo.

Simba imeamua kuchukua hatua hiyo kufuatia hivi karibuni kuachana na kocha wake Zoran Maki ambaye amedumu katika kipindi cha miezi mitatu ndani ya klabu hiyo.

Kikosi hiko kinakwenda kwenye mchezo huo, huku kikiwa na kumbukumbu ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Kmc uliopigwa siku ya jana kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa, Mgunda atakuwa na kikosi hiko mpaka pale mchakato wa kumpata kocha mkuu utakapo kamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!