Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Mgunda atoa tahadhari kwa Mayele kesho
Michezo

Mgunda atoa tahadhari kwa Mayele kesho

Juma Mgunda
Spread the love

 

KOCHA Mkuu wa kikosi cha Coastal Union ya Tanga, Juma Mgunda amesema kwenye mchezo wa kesho wa fainali dhidi ya Yanga, hawatocheza na mshambuliaji hatari Fiston Mayele bali watadili na timu nzima. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Arusha … (endelea)

Mchezo huo wa fainali utapigwa kesho kwenye dimba la Sheikh Amri Abeid jijini Arusha majira ya saa 9:30 jioni.

Wakati akiongea na waandishi wa Habari jijini Arusha, Mgunda alisema kuwa kwenye mchezo huo wao wanaenda kupambana na Yanga na sio kumuangalia mchezaji mmoja

‘Kwanza. niseme kitu kimoja, hatuchezi na Mayele kesho, tunacheza na Yanga, kama Mayele atakuwa kwenye Yanga tutakutana na Yanga, hautuchezi na mtu,” alisema kocha huyo.

Katika michezo yote miwili ya Ligi Kuu waliokutana kati ya Yanga na Coastal Union, Mayele alifanikiwa kuifunga timu hiyo mabaop 2-0, huku mchezo wa mwisho ukiwa wa kutangazwa ubingwa.

Katika hatua nyingine kocha huyo kuelekea mchezo huo amefunguka kuwa wanawaheshimu Yanga na wamejiandaa na mchezo wa kesho kwa kutambua ubora wa mpinzani wao.

“Tumejiandaa kwa mchezo wa kesho na ndio maana tupo hapa na fainali inajulikana lazima mshindi apatikane na maandalizi ya mchezo huo tayari yameshakamalika,” alisema Mgunda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!