TAREHE 6 Septemba 2021, mwaka huu ulimwengu wa soka ulikumbwa na simanzi baada ya mchezaji wa zamani wa Ufaransa, Jean Pierre Adams kufariki dunia. Anaripoti Gabriel Mushi, Dar es Salaam … (endelea).
Licha ya kwamba ni mchezaji wa zamani tena aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73, historia yake na chanzo kilichomsababisha kulala moja kwa moja au kuwa katika hali ya koma kwa miaka 39 ndicho kilichozidisha machungu kwa wafuatiliaji wa soka.
Jean Pierre Adams ni raia wa Ufaransa mwenye asili ya Senegal.
Alizaliwa tarehe 10 Machi 1948 katika jiji la Dakar, nchini Senegal, alipofikisha umri wa miaka 10 akiwa ameambatana na bibi yake alihamia nchini Ufaransa katika kijiji cha Montargis, Loiret.
Bibi yake alikuwa mhudumu wa misheni katika parokia moja ya kanisa katoliki nchini Senegal na alipohamia Ufaransa vivyo hivyo alihudumu katika Parokia ya Loiret.
Fuatilia simulizi ya Adams kujua kile kilichosababisha akakaa kwenye koma kwa miaka 39.
Leave a comment