Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgomo Kariakoo ngoma nzito, wafanyabiashara wamtaka Rais Samia
Habari Mchanganyiko

Mgomo Kariakoo ngoma nzito, wafanyabiashara wamtaka Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

MGOGORO wa kodi katika Soko la Kimataifa la Kariakoo umechukua sura mpya baada ya baadhi ya wafanyabiashara kutishia kuendelea kufunga maduka yao hadi watakapokutana na Rais Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya kupata ufumbuzi wa changamoto zao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamejiri leo Jumatatu, jijini Dar es Salaam, baada ya Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla, kuwataka wafungue maduka hayo ili kupisha mazungumzo kati yao na Serikali, kwa ajili ya kutafuta suluhu.

Makalla alifika sokoni hapo mapema leo, baada ya wafanyabiashara hao kutishia kufunga maduka kwa muda usiojulikana, hadi pale malalamiko yao ya kikodi yatakapofanyiwa kazi.

Makalla aliagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), isitishe operesheni zake sokoni hapo kwa muda hadi ufumbuzi wa mgogoro huo utakapopatiwa ufumbuzi.

Pia aliagiza uongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo, kuunda timu itakayokwenda kuzungumza na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, tarehe 18 Mei 2023, jijini Dodoma.

Licha ya maagizo hayo wafanyabiashara wengi walionesha kutoridhishwa nayo wakidai hayatafanyiwa kazi kwa kuwa sio mara ya kwanza kutolewa.

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania, Ghalib Suleiman, amesema kama malalamiko ya wafanyabiashara wa Kariakoo hayatatatuliwa, mgomo huo utasambaa nchi nzima.

Baadhi ya maduka ya Kariakoo yakiwa yamefungwa

“Kariakoo ndio Tanzania na kitovu cha Biashara nchini, jambo lolote linaanza kwa wakubwa, nyie mnawapa machaguzi wenzenu mkisema kufunga maduka nchi nzima wafanyabiashara wako tayari hata kuhamia Dodoma kwa ajili ya kuzungumza na Rais,” amesema Suleiman.

Katibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo, Peter Mbilinyi, amesema wamemua kuchukua uamuzi wa kufunga maduka kutokana na vilio vyao kutosikikizwa, hususan oparesheni zinazofanywa mara kwa mara na TRA sokoni hapo, ambazo zimesababisha wateja wao hasa wa kutoka nje ya nchi, kuwakimbia.

Pia, Mbilinyi amesema sababu nyingine ya mgomo huo ni kodi mpya ya maghala ya kuhifadhia mizigo.

Mjumbe wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo, Honest Kalist, alisema “hapa hakuna kurudi nyuma, hili suala ili liishe salama na wafanyabiashara kufikia malengo Yao inabidi wakutane na Rais, sababu wasaidizi wake wamefika bila mafanikio.”

Mfanyabiashara Bernard Kalumba, alisema wanataka kuzungumza na Rais Samia kwa kuwa wasaidizi wake walishazungumza nao bila mafanikio.

“Makubaliano yetu katika group ni kwamba tunataka kusikilizwa na Rais Samia, kwa Nini tunataka kusikilizwa nae, kwa sababu hawa wasaidizi wake tulishaongea naye akiwemo Waziri wa fedha akasema hakuna mizigo itakayokamatwa lakini hakuna mafanikio yoyote mizigo inaendelea kukamatwa,” amesema Kalumba.

Amos Makala, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam

Baadhi ya wafanyabiashara hao wameweka ahadi ya kuwazuia wenzao watakaojaribu kufungua maduka yao.

Kufuatia maoni hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Mbwana aliwataka wafanyabiashara wafanye wanachokitaka, baada ya jitihada zake za kuwatuliza kugonga mwamba.

Hadi MwanaHALISI Online inaondoka eneo la tukio, asilimia kubwa ya wafanyabiashara walikuwa wamefunga maduka yao, huku wafanyabiashara wadogo (wamachijga) wakiendelea kufungua meza zao.

Mtandao huu ulipozungumza na baadhi ya wamachinga sababu zao wao kuendelea na biashara, walijibu “hao wanaogoma ni wakubwa, watajijua wenyewe. Sisi tuna familia watoto Wetu hawali mpaka tuingie barabara, wenzetu wanaogoma wanahela.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!