Spread the love
TOKYO Sexwale, ambaye ni Mgombea wa urais wa Fifa kutoka Afrika Kusini amejiondoa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa mrithi wa Sepp Blatter.
Sexwale, akihutubu kabla ya kura kupigwa, amesema hataki kugawanya kura na akawahimiza wajumbe waamue kati ya wagombea wanne waliosalia.
Ameahidi kuunga mkono na kufanya kazi na atakayeshinda. “Nafikisha kampeni yangu kikomo hapa,” amesema.
Wagombea waliosalia ni Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa, Gianni Infantino, Mwana mfalme Ali bin al-Hussein, na Jerome Champagne.
More Stories
Yanga yapigwa tatu na Simba, yashushwa kileleni
Mshambuliaji Dodoma jiji ashinda tuzo
Katwila awabwaga Makata, Simkoko tuzo VPL