Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Mgombea Urais azomewa nyumbani kwake
HabariHabari Mchanganyiko

Mgombea Urais azomewa nyumbani kwake

Spread the love

KIONGOZI wa chama cha Wiper nchini Kenya, Kalonzo Musyoka, amekutana na udhalilishaji akiwa jukwaani baada ya kundi kubwa la wananchi wanaomsikiliza kumzomea akifanya kampeni katika kaunti yake ya nyumbani ya Kitui jana tarehe 17 Juni, 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kalonzo alilazimika kuvumulia hali hiyo katika soko la Ikutha nchini humo alipozomewa mara kadhaa na kulazimika kukatiza hotuba yake.

Umati huo uliotamka ‘kwenda huko’ ulikuwa ukipinga juhudi zake za kumfanyia kampeni mbunge wa Kitui Kusini na mgombea wa chama cha Jubilee, Racheal Kaki Nyamai na kusisitiza kuwa mgombea wa ODM, Onesmus Mumo King ndiye awe mzumngumzaji badala yake.

Wakati hayo yakiendelea, Mgombea mwenza wa William Ruto kupitia tiketi ya UDA Rigathi Gachagua naye alipagwa butwaa alipokuwa akifanyia kampeni ya Muungano wa Kenya Kwanza katika eneo la Githunguri, Kaunti ya Kiambu.

Gachagua alipata wakati mgumu kutuliza umati baada ya kuwashambulia Rais Uhuru Kenyatta na Azimio La Umoja One na mgombea urais wa chama cha Muungano wa Kenya, Raila Odinga.

Baadhi ya umati ambao haukutaka kusikia lolote walielezea kukerwa kwao na mashambulizi yake dhidi ya wawili hao na kumshutumu kwa kutomuheshimu rais na Raila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!