Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgogoro wafanyabiashara sabasaba Dodoma wahitimishwa
Habari Mchanganyiko

Mgogoro wafanyabiashara sabasaba Dodoma wahitimishwa

Naibu Meya wa halmashauri ya Jiji, Emmanuel Chibago
Spread the love

 

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma, nchini Tanzania, limemaliza mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 20 kati ya halmashauri hiyo na wafanyabiashara wa soko la Sabasaba. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mgogoro huo umepatiwa ufumbuzi baada ya Naibu Meya wa halmashauri ya Jiji, Emmanuel Chibago na Afisa Biashara wa Jiji, Donatila Vedasto kukaa vikao vya mara kwa mara ambavyo vilikuwa vikilenga kujenga mahusiano mazuri hususani katika suala zima la ulipaji kodi.

Katika mkutano wa pamoja uliofanyikia katika ofisi ya soko la sabasaba kwa kuwashirikisha viongozi wa Jiji na wafanyabiashara, Donatila alisema, umefika wakati sahihi sasa kwa wafanyabiashara wa soko la sabasaba kulipa kodi kwa faida ya uboreshaji wa soko hilo.

“Ndugu zangu wafanyabiashara wa sabasaba, tumekuwa tukifanya mikutano na vikao mara kwa mara ili kutafuta ufumbuzi wa kulipa kodi ndani ya soko letu la sabasaba.”

“Na kulipa kodi ni pamoja na kujisajili ili kila mfanyabiashara aweze kufahamika na aina ya biashara anayoifanya kwa kufanya hivyo kutasaidia kuwatambua na wale ambao watakuwa wamejisajiri kwa vyovyote vile yanapotokea maboroshe watu hao watapewa kipaumbele tofauti na wale ambao bado hawajajisajiri”alieleza Donatila.

Naye Naibu Meya Chibago, aliwaambia wafanyabiashara hao wa soko la sabasaba ili nchi iweze kupiga hatua ni lazima kodi ilipwe kwa maendeleo ya nchi.

“Wafanyabiashara wa sabasaba tumekuwa tukizungumzia ulipaji wa kodi, ukweli ni hatuwezi kukwepa ulipaji wa kodi katika eneo hill la wafanyabiashara lakini pia uongozi wa halmashauri ya Jiji hauwezi kukaa peke yao na kupanga kodi ambayo mnatakiwa bali kinacho fanyika ni kushirikishana na kufikia mwafaka kama ilivyofanyika katika mkutano huu,” alisema Chibago.

Kwa upande wake, mmoja wa wafanyabiashara, Steven Masawe alisema wafanyabiashara hawana tatizo na ulipaji wa kodi ili mradi tu uwekwe utaratibu unaotakiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!