Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mgogoro wa ardhi waibuka upya Karagwe
Habari Mchanganyiko

Mgogoro wa ardhi waibuka upya Karagwe

William Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Spread the love

MAMIA ya wananchi wa kijiji cha Chabuhora, wilayani Karagwe, mkoani Kagera, wanahitaji msaada wa haraka wa chakula, baada ya mashamba na nyumba zao kuchomwa moto katika kinachoitwa, “operesheni maalum ya mkuu wa wilaya hiyo, anaandika Joseph Sekiku.

Taarifa kutoka Karagwe zinasema, mkuu huyo wa wilaya aliamua kuchomwa moto nyumba na  mashamba hayo ya wananchi, kwa madai ya kutaka kuwabeba wafugaji.

Taarifa zinasema, wananchi wanaoishi katika maeneo hayo, wamekuwapo kwa miaka kadhaa sasa; wanamiliki maeneo hayo kwa kibari cha serikali ya kijiji.

“Lakini mkuu wa wilaya amefika hapa. Ameanza kuchoma moto nyumba za wananchi na kuwahamisha kwa nguvu.

Anadai sisi ni wavamizi, wakati tumemilikishwa maeneo hayo na serikali za kijiji na tumekuwapo hapa tangu enzi na enzi,” ameeleza mzee mmoja wa makamo kwa sharti la kutotajwa jina.

Anasema, serikali  wilayani humo imekuwa ikidai kuwa wananchi hao wameondolewa katika maeneo hayo kutokana na kuvamia vyanzo vya maji.
Anasema, “serikali ya kijiji imetoa ardhi kwa kaya zile ili waishi na walime.

Hata stakabadhi wanazo. Lakini sasa wameondolewa katika eneo hilo na kuwacha wapweke. Mvua za masika zimeanza na wananchi hawa hawana pa kulala na hawana chakula.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Ditopile aungana na Wana-Kongwa kwa Iftar, wamuombea dua Rais Samia

Spread the loveKATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti...

Habari Mchanganyiko

PSSSF yawekeza kwenye viwanda 4, kuzalisha ajira 3,000

Spread the loveKATIKA kuisaidia Serikali kupunguza tatizo la uhaba wa ajira nchini,...

Habari Mchanganyiko

Luhemeja ahimiza utunzaji rasilimali maji kwa faida ya vizazi vijavyo

Spread the love  NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja...

Habari Mchanganyiko

NSSF yawapa darasa wahariri uwekezaji wa nyumba, yapewa cheti

Spread the loveMFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa wito...

error: Content is protected !!