ASKOFU Mkuu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dk Steven Munga, amewakingia kifua wachungaji sita.
Hao ni waliosimamishwa kazi ya kutoa huduma kwenye Dayosisi hiyo, kwa madai ya “ubadhirifu wa fedha.”
Jana, Askofu Munga alisema, madai kuwa wachungaji hao, ni wabadhirifu wa mali za Kanisa, hayana ukweli na kwamba kuibuka kwa tuhuma hizo sasa, ni mwendelezo wa makundi ya uchaguzi wa kiongozi wa Dayosisi hiyo.
“Ninawafahamu vizuri sana. Nimetumika nao kwa miaka mingi. Wana uadilifu wa hali ya juu na hoja nzuri na zenye mantiki. Niko nyuma yao,” alieleza Askofu Dk Munga.
Soma zaidi habari hii katika Gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Jumanne, tarehe 7 Desemba 2021, kujua alichokisema Askofu Muga, waliosimamishwa pamoja na majibu ya Askofu Mbilu anayenyooshewa kidole kuhusika katika mgogoro huo.
Leave a comment