Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgawo wa maji wamuibua Prof. Lipumba, amtahadharisha Rais Samia
Habari Mchanganyiko

Mgawo wa maji wamuibua Prof. Lipumba, amtahadharisha Rais Samia

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameishauri Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuja na mipango endelevu ya kutumia mabonde ya maziwa na mito, kuzalisha maji ya kutosha kwa ajili ya kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma hiyo muhimu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na wanahabari, leo Jumanne, jijini Dar es Salaam, Profesa Lipumba amesema nchi ina mabonde makubwa tisa, lakini Serikali imekosa mikakati madhubuti ya kuyatumia katika kuzalisha maji.

“Ukitazama takwimu ya uzalishaji maji na mahitaji ya maji, unakuta uzalishaji ni mdogo kuliko mahitaji. Mfano uzalishaji wa maji wa Dawasa kwa 2021 ilikuwa lita za ujazo milioni 147, wakati mahitaji ambayo yalikadiriwa 2020 yalikuwa lita za ujazo milioni 207 hivyo uzalishaji ulikuwa asilimia 70,” amesema Prof. Lipumba.

Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba

Mbali na matumizi sahihi ya mabonde ya maji, Prof. Lipumba ameishauri Serikali kuweka utaratibu mzuri wa kuvuna maji ya mvua na yale yaliyoko chini ya ardhi.

Katika hatua nyingine, Profesa Lipumba amemtahadharisha Rais Samia kuwa, kama changamoto ya uhaba wa maji iliyopo sasa haitatafutiwa ufumbuzi hadi Oktoba 2025, wananchi watashindwa kupiga kura kwa sababu ya kutafuta maji.

“Lazima tuwe na mikakati endelevu na Rais anaweza kulijua hili vizuri kabisa sababu ukiwa unaingia 2025 Oktoba, ndiyo uchaguzi unafanyika watu wakiwa na ndoo kichwani wakashindwa kupiga kura kisa wanatafuta maji, hali haitakuwa nzuri. Suala hili si dogo ni la maisha ya watu lakini lina athari zake katika hali ya siasa,” amesema Prof. Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!