KUKOSA kiungo kimoja katika mwili wako ama kuwa na ulemavu sio mwisho wa maisha. Anaripoti Hamis Mguta, Iringa…(endelea).
Kauli hii inathibitishwa na mgahawa maarufu wa Neema Craft uliopo mkoani Iringa nchini Tanzania, ambao umeajiri watu wenye ulemavu wa kusikia (viziwi).
Riziki Mgimba, mfanyakazi katika kituo hicho anasema, wahudumu wote pamoja na wapishi katika mgahawa huo ni viziwi na wana uwezo wa kuhudumia wateja bila tatizo.
MwanaHALISI TV, limeweka nanga katika mgahawa huo nakuzungumza naye mengi kuhusu namna wanavyohudumia watu, na sababu ya kuajiri viziwi watupu kwenye mgahawa huo..
Tazama video hapa chini kujua zaidi…
Leave a comment