Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mgahawa maarufu Hong Kong wazama
Kimataifa

Mgahawa maarufu Hong Kong wazama

Spread the love

 

MGAHAWA kutoka Hong Kong uliofanya kazi takribani miaka 50 , umezama siku chache baada ya kuvutwa kutoka bandarini. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).

Jumba hilo lilitumbukia katika Bahari ya Kusini ya China wakati likielekea eneo lisilojulikana,kampuni mama inayomiliki mgahawa huo, Aberdeen Restaurant Enterprises imeripoti kuwa imehuzunishwa na tukio hilo sana , lakini wanashukuru hakuna wafanyakazi waliojeruhiwa.

Hata hivyo, mgahawa huo ulifungwa machi mwaka 2020 wakati wa janga la Covid 19 liliposhamiri.

Zaidi ya wageni milioni 3 wanaaminika kula vyakula katika hoteli hiyo, kwa miaka minginsana wakiwemo Malkia Elizabeth, Tom Cruise pamoja na Richard Branson.

Pia umeigiziwa filamu kadhaa ikiwa ni pamoja na filamu ya Bond, lakini janga la corona lilifanya biashara hiyo kuwa mbaya zaidi baada ya wageni kutotembeleapo tena.

Aidha meli hiyo ilipaswa kukaa katika eneo lisilojulikana huku ikisubiria mwendeshaji mpya.

Lakini ilizama siku ya jumapili tarehe19 juni 2022, karibu na Visiwa vya Paracel baada ya kukabiliana na hali mbaya , nakuanza kuingiza maji Aberdeen Rastaurant Enterpris ilisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!