Hayo yamesemwa leo jijini hapa na Mkurugenzi wa takwimu za uchumi ,Ofisi ya taifa ta takwimu, Daniel Masolwa wakati akitoa taarifa ya mfumko wa bei wa mwezi unaopima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.
Akitoa taarifa hiyo Masolwa alisema mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2019 imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2019.
Pamoja na hayo Mkurugenzi huyo alisema kuongezeka kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi cha mwaka ulioishia mwezi Juni, 2019 zikilinganishwa na bei za mwaka ulioishia mwezi Juni 2018.
“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa mwezi Juni 2019 ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 3.6, samaki wabichi asilimia 27.3, unga wa ngano kwa asilimia 4.4 na mtama kwa asilimia 4.9,” alisema Masolwa.
Aidha alizitaja bidhaa zisizo za chakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa mwezi Juni 2019 kuwa ni pamona na dizeli kwa asilimia 11.4, petroli kwa asilimia 4.9, gharama za kulala kwenye nyumba za wageni kwa asilimia 5.8 na vitabu vya shule kwa asilimia 2.4.
Pamoja na mambo mengine, Mkurugenzi huyo wa takwimu za uchumi aliongeza kuwa mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2019 umeongezeka hadi kufikia asilimia 2.3 kutoka asilimia 2.2 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2019.
“Hata hivyo kwa hali ya mfumuko wa bei kwa nchi za Afrika mashariki kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2019 nchini Uganda umeongezeka hadi asilimia 3.4kutoka asilimia 3.3,” alisema.
Pamoja na hayo alisema,kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2019 umeongezeka hadi asilimia 5.70 kutoka asilimia 5.49 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2019
Leave a comment