Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfumuko wa bei wapanda – Serikali
Habari Mchanganyiko

Mfumuko wa bei wapanda – Serikali

Dk. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

SERIKALI imeeleza kuwa mfumuko wa bei wa taifa, umeongezeka kwa asilimia 0.2 kutoka asilimia 3.4 Septemba hadi asilimia 3.6 Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Dk. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango leo tarehe 13 Novemba 2019, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali lililohoji, mkakati wa serikali katika kudhibiti changamoto ya mfumuko wa bei katika bidhaa muhimu, hasa vyakula.

“Ni sahihi kabisa mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioshia mwezi Oktoba mwaka 2019 umeongezeka hadi asilimia 3.6,  kutoka asilimia 3.4 kwa mwaka ulioshia mwezi Septemba 2019,” ameeleza Dk. Kijaji.

Dk. Kijaji amesema kilichopelekea mfumuko wa bei kuongezeka hasa katika bidhaa za vyakula aina ya unga wa mahindi na maharagwe, ni  baadhi ya maeneo hapa nchini kutopata chakula cha kutosha.

“Nna katika bidhaa zilizochangia ongezeko hili la asimia 0.2 ni bidhaa za chakula, kama taifa tunafahamu hatuna upungufu wa chakula. Tuna chakula cha kutosha, lakini yako maeneo ndani ya taifa letu ambayo hayakupata chakula cha kutosha, na hivyo yamepelekeea kuongeza bei ya bidhaa hizi,” amesema Dk. Kijaji.

Kufuatia changamopo hiyo, Dk. Kijaji amesema Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) imeanza kutoa chakula kwa bei nafuu katika maeneo yenye upungufu wa chakula, ili kupunguza bei ya bidhaa hizo.

“Kama taifa tunalitambua hili, na tayari NRFA wameshatoa angalizo kutoa chakula hiki kwa wafanyabishara.

“Wanunue kwa bei nafuu ili kupeleka maeneo ambayo yana upungufu, na hatimaye kupunguza bei ya chakula na taifa letu ya kuwa na mfumuko wa bei mdogo na watanzania kupata chakula na bidhaa nyingine kwa bei rahisi na wanazozimudu,” amesema Dk. Kijaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!