MFANYABIASHARA Yusuf Manji na wenzake watatu wamezidi kusota rumande baada ya kesi yake kupigwa kalenda hadi Agost 9, mwaka huu, anaandika Faki Sosi.
Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Mkazi Kisutu, Huruma Shahidi na Wakili wa serikali Kisenyi Mutalemwa, aliomba tarehe nyingine ya kuitaja kwa kuwa ushahidi haujakamilika.
Manji na wenzake walifikishwa kizimbani kwa tuhuma za kukutwa na sare jeshi pamoja na tuhuma nyingine zinazohusu masuala ya usalama wa nchi.
Leave a comment