Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya wa Chadema Iringa ang’olewa
Habari za Siasa

Meya wa Chadema Iringa ang’olewa

Alex Kimbe, aliyekuwa Meye wa Iringa
Spread the love

ALEX Kimbe, Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo tarehe 28 Machi 2020, ameondolewa madarakani na Baraza la Madiwani la halmashauri hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Hatua hiyo imechukuliwa katika kikao maalumu cha baraza la madiwani kilichoketi leo, kwa ajili ya kujadili tuhuma zilizokuwa zinamkabili Meya Kimbe, ikiwemo za matumizi mabaya ya madaraka na mamlaka.

Meya Kimbe ameondolewa madarakani kwa kura za ndio 14 kati ya 26, zilizopigwa na wajumbe katika kikao hicho.

Kwa mujibu wa Hamid Njovu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Meya Kimbe ameondolewa madarakani, baada ya Tume ya Uchunguzi dhidi yake iliyoundwa na Ally Hapi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, kumkuta na hatia.

Njovu amedai kuwa, Meya Kimbe aliamuru baadhi ya wajumbe wa halmashauri hiyo, kufanya ziara mkoani Mbeya na Njombe, pasipo kupata kibali cha Mkuu wa Mkoa.

“Amekuwa akitumia nafasi yake vibaya ya madaraka na mamlaka, matokeo ya uchunguzi ni kama ifuatavyo, kuamuru wajumbe wa halamshauri kufanya ziara pasipo kupata kibali cha mkuu wa mkoa,” amedai Njovu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!