Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Mwanza akamatwa asimwage mboga mbele ya Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Meya Mwanza akamatwa asimwage mboga mbele ya Rais Magufuli

Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire. Picha ndogo, Kiomoni Kibamba, Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza
Spread the love

MEYA wa Jiji la Mwanza, James Bwire amekamatwa na jeshi la Polisi muda mchache kabla ya kutoa salamu zake kwa Rais John Magufuli katika uzinduzi wa kiwanda cha Sayona kwa kuhofia kutoa siri ya ufisadiwa ujenzi wa kiwanda hicho, anaandika Mwandishi Wetu.

Tukio hilo limetokea baada ya kubainika katika salamu za Meya kwa Rais Magufuli, kulikuwa na maelezo ya ufisadi wa kiwanda hicho kilichopo Nyakato Ilemela jijini Mwanza.

Wanaotajwa kufanya ufisadi huo ni mkurugenzi wa Jiji hilo, Kiomoni Kibamba na viongozi wengine wa mkoa huo.

Pia viwanda vya kampuni hiyo vimekuwa vikituhumiwa kuwanyanyasa wafanyakazi wake wengine wakitimuliwa kazi bila kulipwa stahiki zao.

Baada ya kamati ya Ulinzi na usalama mkoa wa Mwanza chini ya John Mongella kubaini kwamba Meya huyo anataka kumwaga ukweli mbele ya rais, inadaiwa aliliagiza jeshi la Polisi kumkamata kiongozi huyo ambaye kwa kipindi kifupi ameonekana akifichua uchafu unaofanyika katika jiji la Mwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!