Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Jacob kama Lissu,  amparura Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Meya Jacob kama Lissu,  amparura Magufuli

Spread the love

BONIPHACE   Jacob, Mstahiki Meya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaama amemtaka Rais John Magufuli, Rais wa Jamuhuri ya Muungano  kuwakemea watendaji wa serikali wanaokataa kupeleka maendeleo kwenye maeneo ambayo wapinzani walishinda uchaguzi, anaandika  Irene Immanuel.

Boniphace ameyasema hayo leo huku akisema kumekuwapo na uwezeshaji hafifu wa maendeleo katika maeneo ambayo wapinzani wanayaongoza.

“Mmoja ya mtu tunaye mlalamikia sana kuwa mstari wa mbele kukwamisha miradi kwenye maeneo yanayoongozwa na  wapinzani ni aliyetajwa na Tundu Lissu, kama ndugu wa karibu wa Rais (mpwa wake),”  amesema

“Doto James akiwa Naibu katibu mkuu wizara ya fedha na mipango ndiye alikwamisha mradi wa kujengewa kiwanda cha mbolea, kule Mabwepande.” amesema

Amesema wakati akiwa Meya wa Kinondoni, alifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wananchi wake wanapata maendeleo, lakini James alisababisha kunyimwa ufadhili wa kiwanda chenye thamani ya Sh. bilioni 3.2 kutoka kwa serikali ya Ujerumani.

Alimtaja  James kuwa ndiye anayelalamikiwa na Bella Bird, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa kuchelewesha kwa makusudi mradi wa uboreshaji wa jiji la Dar es salaam kwa halmashauri zote za wapinzani.

Amesisitiza umuhimu wa Rais John Magufuli, kujitokeza hadharani  kuwakana au aseme kawatuma wote wanaokwamisha miradi kwenye halmashauri za wapinzani huku akiwataka wananchi kutokubali ubaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!